SEHEMU
YA 1: UTANGULIZI
Dubbing
Development Group (DDG)
ni kikundi cha wasanii wanaonakirisha sauti waliokusudia kuunganisha nguvu
zao pamoja ili kupambana na umaskini na hatimaye kuongeza kipatao kupitia
shughuli mbali mbali za kisanaa na ujasiliamali. Kikundi kimeanzishwa
kikiwa na wanachama waliolenga kujiletea maendeleo, hivyo kuweza kukidhi
mahitaji ya msingi ya wanachama katika shughuli za maendeleo
IBARA YA 1: JINA LA KATIBA
Katiba hii inajulikana kama
‘katiba ya kikundi cha DUBBING DEVELOPMENT GROUP kilianzishwa
mwaka 2019.
SEHEMU
2: JINA, ANUANI YA KIKUNDI
IBARA YA 2: JINA LA KIKUNDI
Kikundi kinajulikana kwa
jina la DUBBING DEVELOPMENT GROUP. Kwa kifupi D.D.G
IBARA 3: OFISI NA ANUANI YA
KIKUNDI
Ofisi na Makao makuu ya
kikundi yapo Nyumba namba……………… mtaa…………………. kata ya …………… Wilaya ya ………………….,
Anuani ya posta S.L.P ……….
Kinondoni, Mkoa wa Dar es salaam.
IBARA YA 4: ENEO LA
SHUGHULI ZA KIKUNDI
Shughuli za kikundi
zitafanyika Tanzania nzima bara na visiwani
IBARA YA 5: LUGHA
Lugha inayotumika ni kiingereza
na Kiswahili.
SEHEMU
YA 3: MADHUMUNI YA SHUGHULI ZA KIKUNDI
IBARA 6: MADHUMUNI YA
KIKUNDI
a) Kuwezesha
wanachama kujikwamua kiuchumi
b) Kuanzisha
msingi wa kuwa na vyanzo vingi vya mapato ili kujiongezea kipato.
c) Kukopeshana
fedha yenye masharti nafuu
d) Kushirikiana
na kusaidiana katika raha na shida.
IBARA YA 7: SHUGHULI ZA
KIKUNDI
a) Kushirikiana
na kusaidiana
b) Kuelimisha
wanachama elimu ya biashara na ujasiliamali
c) Kulinda
na kutetea maslani ya wasanii wanakilisha sauti Tanzania(Dubbing artist)
SEHEMU
YA 4: UANACHAMA
IBARA 8: TARATIBU ZA
UANACHAMA.
Kikundi kitakuwa na wanachama waanzilishi ambao watakuwa ndio waliounda wazo hili kwa pamoja ambao wamekidhi vigezo na sifa ya kuwa wanachama. Idadi ya wanachama inaweza kuongezeka kadri wanachama wapya watakavyojitokeza.
IBARA 9: AINA YA WANACHAMA
a) Kutakuwa
na wanachama waanzilishi ambao wameshiriki kuandaa katiba hii na wamelipa
kiingilio cha Tshs 50,000/=
b) Kutakuwepo
na wanachama walezi iwapo wanachama wataona umuhimu wa kufanya hivyo.
c) Wanachama
watakaoingia baada kikundi kuundwa watapaswa kulipa kiingilio cha shilingi
50,000/= Pamoja na jumla ya michango yote iliochangwa na wajumbe wengine
IBARA 10: SIFA YA UANACHAMA
Mtu yeyote anaweza kuwa
mwanakikundi anapokuwa na sifa zifuatazo: -
a)
Awe mtu anayehusiana na sanaa za
unakirishaji sauti
b)
Awe mwenye kutunza siri za kikundi.
c)
Awe na umri wa miaka 18 na kuendelea.
d)
Awe anakubaliana na masharti ya katiba hii
na kuifuata.
e)
Awe ameshiriki kikamilifu katika shughuli za
uchumi zinazoendeshwa na kikundi.
f)
Awe na akili timamu.
g)
Awe mwenye tabia njema, anayejituma na
anayejiheshimu.
h)
Awe mwenye uelevu yakinifu unaokusudia
maendeleo.
i)
Awe mchapa kazi na mbunifu.
j)
Awe mwaminifu.
IBARA 11: HAKI ZA
MWANACHAMA
a)
Kugombea uongozi na kuchaguliwa au kuchagua
viongozi anaowaona wanafaa.
b)
Kujieleza na kujitetea anaposhutumiwa hatua
kwa hatua mbele ya kamati ya utendaji, mikutano ya kikundi au uongozi wa
serikali.
c)
Kupata taarifa zote za masuala ya kikundi na
kuhoji maendeleo ya kikundi.
d)
Kupewa hadhi na huduma sawa na wenzake bila
upendeleo.
e)
Kupata mkopo pindi atakapohitaji.
f)
Kila mwanakikundi anayo haki ya kupewa gawio
sawa na mapato ya kikundi na taratibu za kikundi.
g)
Kukemea ukiukwaji wa kanuni na taratibu za
katiba kwa viongozi
IBARA 12: WAJIBU WA
MWANACHAMA
Wanakikundi wote watakuwa
na wajibu na majukumu yafuatayo: -
a)
Kuhudhuria na kushiriki katika vikao vyote
halali kwa mujibu wa katiba.
b)
Kutoa michango yote halali kama
ilivyoanishwa na katiba pamoja na michango mingine itakavyokubaliwa na
wanachama kwenye vikao kwa wakati.
c)
Kuheshimu na kutekeleza maagizo halali
kwenye vikao.
d)
Kushiriki kikamilifu katika shughuli zote
halali na kuongeza kipato.
e)
Kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha
kikundi.
IBARA YA 13: UKOMO WA
MWANACHAMA
Mwanakikundi atakoma kuwa
mwanachama kwa:-
a)
Kifo.
b)
Kufukuzwa kwa utovu wa nidhamu.
c)
Kutolipa michango na hisa kwa kipindi cha
miezi sita mfululizo bila ya sababu maalumu.
d)
Kutohudhuria vikao vitatu mfululizo bila ya
taarifa.
e)
Kushindwa kushiriki kikamilifu katika
shughuli za kiuchumi za kikundi mfano miradi ya kikundi.
f)
Kupata ugonjwa wa akili utakaothibitishwa na
Daktari.
g)
Kujiuzuru mwenyewe kwa hiari yake.
IBARA 14: ADA YA MICHANGO
YA WANACHAMA
a) Kila
mwanachama mpya anatakiwa kulipa ada ya kiingilio cha Tshs 50, 000/=
b) Kila
mwanachama atatakiwa kulipa michango mingine iliyoanishwa na kukubaliwa na
wanachama wote.
c) Kila
mwanachama anatakiwa kulipa Hisa, thamani ya hisa moja itapangwa na kukubaliana
na wanachama wote. Kiwango cha chini cha kununua hisa kuanzia hisa 1 na kiwango
cha juu ni hisa 10. Mwanachama anaweza kutanguliza ununuzi wa hisa za ziada
lakini asidaiwe hisa za nyuma.
d) Kila
mwanachama analazimika kuchangia Tshs 2500/= kwa wiki kama mchango wa mfuko wa
jamii na elimu.
e) Kila
mwanachama atalazimika kuchangia kiasi cha pesa kitakachopangwa kwa ajili ya kumsaidia
mwanachama mwenzetu atakayepata dharula pale inapobidi.
f) Michango
na ada itafanyika kupitia vikao vya vikundi.
IBARA 15: FAIDA
ZITAKAZOPATIKANA
a) Kujikwamua
kiuchumi.
b) Kumwezesha
mwanachama kupata fedha kwa ajili ya matumizi yake.
c) Kujenga
uwezo wa kujiongezea kipato kwa wanakikundi.
SEHEMU
YA 5: MUUNDO WA MAJUKUMU YA UONGOZI.
IBARA 16: UONGOZI WA
KIKUNDI
Kikundi kitakuwa na uongozi
ambao utasimamia shughuli zote zilizopo ndani ya kikundi kitakuwa na uongozi
kwa mtiririko ufuatao:-
1.
Mwenyekiti.
2.
Katibu.
3.
Mweka hazina.
4.
Wajumbe watano
IBARA YA 16: 1: MAJUKUMU YA
MWENYEKITI
Mwenyekiti atakuwa na
majukumu yafuatayo:-
a)
Kusimamia/kuongoza mikutano ya kikundi.
b)
Kuweka sahihi kwenye fomu za mikopo na
nyaraka za kikundi kwa ujumla.
c)
Kuitisha mikutano yote mikuu ya kikundi.
d)
Ni msemaji mkuu wa kikundi.
e)
Kukiwakilisha kikundi nje ya kikundi.
f)
Kujibu maswali na kutoa maelezo juu ya mambo
mbali mbali katika mkutano mkuu.
IBARA 16: 2: MAJUKUMU YA
KATIBU
Katibu atakuwa na majukumu
yafuatayo:-
a)
Ni mtendaji/ mtekelezaji mkuu wa shughuli za
kikundi.
b)
Mwenye kutunza na kuhifadhi kumbukumbu za
kikundi.
c)
Kumshauri mwenyekiti katika kazi za kila siku.
d)
Kuandaa kumbukumbu zote muhimu za kikundi
pamoja na kumbukumbu za kifedha.
e)
Kufanya mawasiliano na wafadhili ( Serikali,
Taasisi, NGOs, CBOs n.k)
f)
Kuitisha mikutano na kuandaa kama
atakavyoagizwa na mwenyekiti.
g)
Kutekeleza maamuzi ya uongozi na mikutano ya
wanakikundi.
h)
Ataweka sahihi kwenye fomu za mikopo na
nyaraka nyingine za fedha na mali za kikundi kwa ujumla.
IBARA 16: 3: MAJUKUMU YA
MWEKA HAZINA.
Mweka hazina atakuwa na
majukumu yafuatayo:-
a)
Kutunza kumbukumbu zote ambazo zinahusu
fedha za kikundi.
b)
Kupokea fedha na kuzitunza au kuziwasilisha
zinapohusika kwa mujibu wa katiba na maelekezo wa wanakikundi.
c)
Kuandaa na kuwasilisha taarifa za fedha
kwenye mkutano mkuu na kutoa ushauri wa matumizi ya fedha.
d)
Kufanya shughuli zote za fedha ambazo
atapangiwa na kikundi ikiwa na pamoja na kuweka sahihi kwenye hundi na nyaraka
nyingine za fedha.
IBARA YA 17: KAMATI TENDAJI
Kamati hii itafanya kazi
mbalimbali za kikundi na itakuwa na wajumbe wafuatao:-
1.
Mwenyekiti.
2.
Katibu.
3.
Mweka hazina.
4.
Wajumbe watano miongoni mwa wanakikundi na kufanya
kamati kuwa na wajumbe 8.
NB:
Kamati hii inaweza kubadilika kutokana na ongezeko la wanachama.
IBARA 17: 1: MAJUKUMU YA
KAMATI TENDAJI
a)
Kushughulikia na kuandaa mipango ya
maendeleo ya kikundi.
b)
Kupokea na kujadili utekelezaji na maazimio
ya mikutano yote ya kikundi.
c)
Kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya mkutano
mkuu na shughuli zote za kikundi.
d)
Kubuni na kupendekeza miradi na mbinu
mbalimbali ya kuongeza pato la kikundi.
e)
Kushughulikia masuala yote ya mikopo na
kuwasilisha taarifa hizo katika vikao vya kikundi.
f)
Kutataua migogoro na kero za kikundi.
IBARA 18: MUDA WA UKOMO WA
UONGOZI
a) Viongozi
watakaochaguliwa watakaa madarakani kwa kipindi cha miaka mitatu (3) tangia kuchaguliwa na wanaweza kugombea
awamu nyingine kwa ridhaa ya wanachama.
b) Kiongozi
atakoma uongozi kwa kufukuzwa, kufariki, kuhama, kufungwa jela, zaidi ya mwaka
mmoja (1), kurukwa na akili ama kujiuzuru mwenyewe.
c) Kuondolewa
na wanakikundi kwa kumpigia kura ya kutokuwa imani naye, maamuzi hayo lazima
yafikiwe na wanakikundi wasiopungua ½
wanachama wote.
d) Kutokuhudhuria
vikao viwili bila taarifa na kukiuka onyo kwa kuendelea kutohudhuria vikaoni.
IBARA YA 19: MISINGI YA
UENDESHAJI UCHAGUZI WA VIONGOZI
a) Majina
ya wagombea yatapendekezwa na wanachama au mwanachama kujipendekeza mwenyewe kwenye
mkutano mkuu wa wanachama wote.
b) Upigaji
kura utakuwa mtu mmoja kura moja na
itakuwa ni siri na atakayepata kura za juu ndio atakuwa kiongozi / mshindi,
endapo kura zitafungamana kura zitarudiwa mpaka apatikane mshindi.
c) Utafanyika
uchaguzi wa kujaza nafasi za uongozi zitakapoachwa wazi [pindi
itakapojitokeza].
d) Nafasi
ilioachwa wazi Kaimu atakaimu kwa siku zisizozidi arobaini baada ya hapo lazima
uchaguzi ufanyike
IBARA 20: MIIKO NA MAADILI
YA VIONGOZI
a)
Kiongozi yeyote haruhusiwi kutumia madaraka
yake kwa kutoa maamuzi ya kumnufaisha yeye binafsi, kutoa upendeleo kwa mtu
yeyote kwa maslahi binafsi au kumkandamiza mtu yeyote.
b)
Ni kosa kwa kiongozi yeyote kutoa au kupokea
rushwa ya aina yeyote kwa ajili ya kutoa huduma kwa mtu yeyote, adhabu yake ni
kumfukuza uongozi.
c)
Asitoe siri za kikundi.
SEHEMU
YA 6: MIKUTANO
IBARA YA 21: MKUTANO MKUU
Kutakuwa na mkutano mkuu
ambao utahudhuriwa na wanachama wote ambao utafanyika mara mbili (2) kwa mwaka.
Taarifa ya mkutano itatolewa ndani ya siku saba (7) kabla ya siku ya mkutano.
Mkutano huu utajadili masuala ya kawaida ya maendeleo na kutatua changamoto za
kikundi zilizoshindwa kufanyiwa kazi na kamati Tendaji. Pia mkutano mkuu ndio
utakuwa na jukumu la kufanya maamuzi yote ya kikundi ikiwemo kupanga bajeti ya
kikundi na kupokea taarifa ya fedha
IBARA 22: MKUTANO WA
KAWAIDA
Kutakuwa na Mkutano wa
kawaida wa wanachama wote utakaofanyika mara moja (1) kwa mwezi kwa lengo la
kuwasilisha ada na michango mingine (jamii) pamoja na kujadili maendeleo ya
kikundi.
IBARA YA 23: MKUTANO WA
DHARULA
Kutakuwa na Mkutano wa
dharula ambao utaitishwa pale itakapobidi au itakapotokea jambo lenye kuhitaji
utatuzi wa haraka wa wanachama.
IBARA
24: UENDESHAJI WA MIKUTANO
Mkutano
tajwa kwenye Ibara ya 21 – 23 itaendeshwa na Mwenyekiti na iwapo hatakuwepo
wajumbe watachagua Mwenyekiti wa muda kutoka kwa wajumbe waliohudhuria. Maamuzi
ya kikao yatakuwa halali iwapo ya theluthi mbili (2/2) ya wajumbe wote waliohudhuria kikao hicho. Iwapo
mahudhurio hayatafika 2/3
kikao kitahairishwa na kuitishwa tena baada ya siku saba na wajumbe
wakaohudhuria na kuridhia maamuzi yatakuwa halali hata kama mahudhurio yatakuwa
hayajafika idadi inayotakiwa.
IBARA 25: VIKAO VYA KAMATI
TENDAJI
Kamati
tendaji itakutana kila mwezi mara moja (1) ili kujadili utekelezaji wa shughuli
za kikundi na maagizo/ maamuzi ya mikutano ya wanachama wote kama inaweza
kukutana wakati wowote inapotokea dharula.
SEHEMU
YA 7: TARATIBU ZA FEDHA NA MALI ZA KIKUNDI
IBARA 26: MWAKA WA FEDHA
Mwaka wa fedha utaanza
mwezi wa 4 (April) hadi mwezi wa 3 (March) ya kila mwaka.
Kikundi kitaamua kugawana
faida au kitaendelea kutunza katika mfuko wa kikundi.
IBARA YA 27: VYANZO VYA
MAPATO
Fedha / mapato ya kikundi
yatatokana na: -
a)
Viingilio na michango ya wanachama.
b)
Mikopo toka Taasisi mbalimbali za fedha.
c)
Zawadi / ruzuku au misaada kutoka kwa
wahisani.
d)
Mfuko wa jamii.
e)
Adhabu na faini kutoka kwa wanachama.
IBARA 28: HIFADHI YA FEDHA
a)
Kikundi kitafungua Akaunti Benki ambayo
itaendeshwa na wanachama.
b)
Uendeshaji wa Akaunti utasimamiwa na
Mwenyekiti, Mweka Hazina na wajumbe wawili.
c)
Kutakuwa na makundi mawili kundi A na kundi
B. Kundi A atakuwa Mweka hazina na Mwenyekiti na kundi B atakuwa wajumbe wawili
ambao ndio watia saini na kutoa fedha Benki. Watu wawili ndio wanaruhusiwa
kutoa fedha, mmoja kutoka kundi A na mwingine kutoka kundi B wakiambatanisha
muhtasari wa kikundi uliosaniwa na Mwenyekiti, Katibu sambamba na mahudhurio ya
wanachama unaoonyesha makubaliano ya kuruhusiwa kufanya hivyo.
IBARA 29: MATUMIZI YA FEDHA
a)
Matumizi yote ya fedha za kikundi lazima
yasizidi mapato na yataidhinishwa na kufanyika kwa utaratibu na kanuni zilizomo
katika katiba hii.
HUDUMA
ZITOLEWAZO NA KIKUNDI
MIKOPO
Mikopo itatolewa kwa
wanachama wa kikundi hiki mara tu baada ya kumaliza mafunzo ya akiba na mikopo.
NB:
MIKOPO YOTE HII ITAJADILIWA NA KUTOLEWA NA KAMATI TENDAJI NA KUWASILISHA
TAARIFA KWA WANACHAMA KATIKA KILA KIKAO CHA KAWAIDA CHA WIKI.
MIKOPO
ITATOLEWA KWA MASHARTI YAFUATAYO:-
(a)
Atajaza fomu ya maombi ya mkopo na
atawasilisha maombi ya mkopo kwa kamati tendaji.
(b)
Mkopo utajadiliwa na wanachama wote wa
kikundi.
(c)
Mwombaji wa mkopo endapo atashindwa kulipa
mkopo, hisa zake zitapunguzwa ili kulipia mkopo.
(d)
Maombi ya mkopo yatajadiliwa na kupitishwa
na wanakikundi wote.
(e)
Mikopo itakaoainishwa kwa madhumuni ya
biashara, na kwa shughuli za kimaendeleo ya jamii kwa ujumla.
(f)
Hakutakuwa na mkopo mwingine utakaotolewa
kwa mkopaji mwingine hadi pale deni la mkopo uliotangulia litakapokuwa
limelipwa.
(g) Mkopo
utatolewa kutokana na foleni ya wakopaji.
IWAPO
MKOPO HAUTARUDISHWA KWA KIPINDI KILICHOWEKWA HATUA ZIFUATAZO ZITACHUKULIWA
DHIDI YA MKOPAJI
a)
Muhusika aitwe na kuhojiwa mbele ya
mkutano wa wanachama wote na atoe sababu zake.
b)
Ataweza kupewa muda wa mwezi mmoja (1)
wa ziada ili aweze kumaliza deni kwa wakati.
c)
Muda wa ziada utakapokwisha na muhusika
hakumaliza malipo basi hisa za mkopaji zitakatwa na kulipa deni
MCHANGO
WA MFUKO WA JAMII
·
Kutakuwa na mfuko wa jamii ambao utachangwa
na wanachama wa kikundi.
·
Mfuko wa jamii utatolewa kwa wiki mara moja.
·
Kima cha mchango kwa kila mwanachama kwa
wiki ni Tshs 2500/=
·
Endapo mwanachama hatalipa mchango wa Mfuko
wa jamii hadi kufikia wiki ya mwisho wa mwezi mchango huo utakatwa katika Hisa
zake.
MATUMIZI
YA MFUKO WA JAMII
Mfuko wa jamii utatumika
kuwapa wanachama watakaopatwa na matatizo yafuatayo:-
Kufariki kwa hawa
wafuatao:-
a) Baba
au Mama Mzazi wa mwanachama atapewa pole ya Tshs 200, 000/=
b) Mume
au Mke wa mwanachama atapewa pole ya Tshs 200,000/=
c) Mtoto
wa kumzaa, mwanachama atachangiwa pole ya Tshs 200,000/=
d) Kufariki
kwa mwanachama wahusika watapewa pole ya Tshs 200,000/= pamoja na kurudishiwa michango yote alioichangwa kwa
warithi wake
MFUKO
WA JAMII HAUTAKOPESHWA ILA UTATOLEWA KWA KUAPA PALE WANACHAMA WATAKAPOPATA MAJANGA
YASIYO TARAJIWA KAMA VILE:-
(a)
Mwanachama akipatwa na ajali au janga lolote
wanakikundi watamchangia ili kumsaidia kwenye changamoto hiyo.
FAINI
ZA MWANACHAMA
(a)
Kutohudhuria kikaoni bila ya taarifa faini
itakuwa Tshs 5000/=
(b)
Kuchelewa kufika kikaoni nusu saa tangu
kikao kianze na haukutoa taarifa faini itakuwa Tshs 1000/=
(c)
Kuongea bila ya ruksa ya mwenyekiti faini
itakuwa Tshs 200/=
IBARA 30: MGAWANYO WA MALI
NA MAPATO
a)
Mali za kikundi ni pamoja na vitu vyote
vinavyohamishika na visivyohamishika, vinavyomilikiwa na kikundi kama vile
fedha na vitendea kazi. Mgao wa mapato utategemea mafanikio ya shughuli za
kikundi na wanachama wake.
b)
Iwapo mwanachama amefariki, tathmini ya mali
na mapato itafanyika na kupewa stahiki zake na kukabidhiwa mrithi wake
atakayekuwa amemteua yeye mwenyewe kabla ya kufariki.
c)
Iwapo kikundi kitavunjika mali zote za
kikundi watagaiwa wanachama baada ya kulipa madeni yote.
d)
Endapo mwanachama atajitoa mwenyewe kwa
hiari yake ada yake atapewa baada ya mgao wa wanachama wengine.
SEHEMU
YA 8: UTATUZI WA MIGOGORO NA UENDESHAJI WA KIKUNDI.
a) Mwanachama
hatatakiwa kutoa lugha ya kuudhi katika mkutano/ vikao dhidi ya wanachama
wenzake.
b) Mwanachama
atakayeshindwa kuhudhuria vikao zaidi ya vitatu bila sababu za msingi atakuwa
amejiondoa / amejifukuza mwenyewe.
c) Mwanachama
haruhusiwi kutoa siri ya kikundi, jambo lolote litakaloamuliwa ndani ya kikao
itabaki kuwa siri.
UTARATIBU
WA KUTATUA MIGOGORO KATIKA KIKUNDI NI:-
1.
Uongozi
wa kikundi ndio wenye jukumu la kushughulikia migogoro yote itakayojitokeza,
iwapo uongozi utashindwa kutatua utakuwepo mjadala wa wazi utakaohusisha
wanachama halali wa kikundi kwa lengo la kutafuta suluhu na mwafaka wa jambo
hilo, na endapo tatizo litaendelea hapana budi suala hilo kulifikisha katika
ngazi nyingine za kiserikali ama za kisuluhisho ili kusaidia kutatua mgogoro
huo.
SEHEMU
YA 9: MAREKEBISHO / MABADILIKO YA KATIBA
Hakuna mtu yeyote mwenye
mamlaka ya kubadili, kupunguza kipengele chochote ndani ya katiba hii. Iwapo italazimika kufanya hivyo kulingana na
wakati na mahitaji ya kikundi, mapendekezo ya kurekebisha au kubadili kipengele
chochote cha katiba yatajadiliwa kwanza na uongozi wa kikundi na watatoa
ushauri wa kurekebisha vipengele vya katiba katika Mkutano Mkuu ambao ndio una
mamlaka ya juu kuidhinisha marekebisho ya katiba hii kwa kupiga kura iwapo
maamuzi hayo yatafikiwa robo tatu (3/4)
ya wanachama wote.
SEHEMU
YA 10: KUVUNJIKA KWA KIKUNDI
Kikundi kinaweza kuvunjika
kwa maoni ya ¾ ya wanachama wote
baada ya kupiga kura katika Mkutano Mkuu wa mwaka au Mkutano wa dharula.
SEHEMU
YA 11: HITIMISHO
Sisi wanachama wa kikundi
cha DUBBING DEVELOPMENT GROUP tunakiri
kwamba tumeshiriki kuandaa katiba hii hivyo tutailinda, kuitetea na kuifuata
kama muongozo wetu katika shughuli zetu za kujiletea kipato kupitia kikundi
chetu. Tunapenda kuthibitisha ushiriki wetu kwa kuambatanisha majina na sahihi
zetu katika katiba hii.